Waliofariki ajali ya lori la mafuta yafikia 75

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Idadi ya watu waliopoteza maisha kwenye ajali ya moto iliyotokea juzi Jumamosi Agosti 10, 2019 mkoani Morogoro nchini Tanzania imefika 75.

Idadi hiyo imeongezeka baada ya wengine wanne kufariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam walikohamishiwa kwa matibabu zaidi.

Hospitali hiyo ilipokea majeruhi 46 kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya matibabu zaidi hata hivyo, saba kati yao wamefariki.

Akizungumza leo Jumatatu Agosti 12, 2019 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano MNH Aminiel Aligaesha amesema kwa sasa idadi ya majeruhi wanaoendelea kupatiwa matibabu ni 39.

“Tumepoteza wenzetu wengine wanne na miili yao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hivyo kama kuna ndugu wa karibu waje kwa ajili ya kuwatambua ndugu zao,” amesema Aligaesha.

Kuhusu hali za majeruhi mkuu huyo wa kitengo cha mawasiliano amesema wanaendelea vizuri na wapo wanaoonyesha matumaini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad