Waziri Hasunga atoa maagizo Simiyu, ‘Tekelezeni haraka mkakati huu’

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji, Japhet Hasunga ameutaka Uongozi wa Mkoa wa Simiyu kuanza mara moja utekelezaji wa mkakati kabambe uliozinduliwa Agosti 3, 2019 kuhusu Bima ya Mazao kwa wakulima.

Ametoa maagizo hayo wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu na kuhudhuriwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kupokea maelekezo yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuhusu mustakabali wa zao la Pamba.

Hasunga amesema kuwa kuanza haraka kwa utekelezaji wa uandikishwaji wa wakulima kutaimarisha uwezekano wa kuboresha maisha ya wakulima ambao katika kipindi kirefu wameumia kupitia majanga mbalimbali wanayokumbana nayo ikiwemo mazao yao kuungua moto ama ukame.
Aidha, ameongeza kuwa uzinduzi wa Bima ya Mazao umefanyika katika mkoa wa Simiyu hivyo mkoa huo unapaswa kuanzisha haraka utekelezaji wake.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka amempongeza Waziri wa Kilimo kwa kipindi cha muda mfupi ameweza kuonyesha dira na mwelekeo chanya katika ukombozi wa sekta ya kilimo nchini.


Mtaka ameongeza kuwa, maamuzi ya wizara ya kilimo inayosimamiwa na Waziri Hasunga ya kuanzisha Bima ya Afya, na Usajili wa wakulima ni miongoni mwa mambo muhimu yatakayoinua sekta ya kilimo nchini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad