Ahukumiwa kwenda jela kwa kutoa lugha chafu dhidi Rais Museveni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanaharakati msomi nchini Uganda, Dkt. Stella Nyanzi amehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja na nusu kwa kosa la kumtolea lugha chafu Rais wa nchi hiyo, Yoweri Kaguta Museveni.

Nyanzi amekutwa na hatia ya unyanyasaji wa kimtandao pamoja na mawasiliano ya udhalilishaji dhidi ya rais Yoweri Museveni na familia yake.

Aidha, kabla ya hukumu hiyo, Dkt. Nyanzi alikataa kumsikiliza hakimu wakati akisoma hukumu dhidi yake na badala yake kufanya vurugu kwa kuvua nguo na kuonesha sehemu ya mwili wake.

Wakati kesi ikiendelea, Dkt. Nyanzi alikataa kuomba dhamana na amekuwa katika gereza kuu la Uganda la Luzira kwa miezi minane tangu akamatwe.

Pia Dkt. amekuwa mtu maarufu sana nchini humo ambaye amekuwa akitumia lugha chafu kuukosoa hadharani utawala wa Rais Museveni kwa kuandika katika mitandao ya kijamii maneno yasiyokuwa na staha kuhusu utawala wa Rais huyo.

Dkt. Nyanzi ambaye ni mtafiti wa masuala ya jamii, kabla ya kuanza kampeni yake ya matusi kupitia kwenye mitandao ya kijamii aliwahi kuwa mhadhiri katika chuo kikuu cha umma nchini Uganda cha Makerere.

Sudan: Mauaji ya wanafunzi yapelekea shule kufungwa nchi nzima
Zimbabwe yakerwa na vikwazo vya Marekani dhidi balozi wake nchini Tanzania
Serikali ya Msumbiji na wapinzani wasaini mkataba wa Amani
Hata hivyo, mashtaka hayo chini ya sheria ya matumizi mabaya ya kompyuta ni jaribio la utekelezwaji wa sheria ya uhalifu wa mtandaoni inayokosolewa na wengi.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad