AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mchezaji raia wa Tanzania Abdi Banda anayecheza nchini Afrika Kusini amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu yake ya Highlands Park inayoshiriki ligi kuu ya nchi hiyo.
Banda ambaye anacheza nafasi ya mlinzi wa kati mshahara wake utakuwa ni rand 150,000 ambazo ni zaidi ya Sh Milioni 24 za Kitanzania.
Kabla ya kusaini ‘dili’ hilo, Banda alikuwa anakipiga Baroka FC ya Afrika Kusini ambayo aliachana nayo baada ya mkataba wake kumalizika.
Ikumbukwe beki huyo kabla ya kutua Baroka alikuwa akiichezea Simba SC ambayo ilimsajili kutokea Coastal union ya Tanga.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK