AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mchekeshaji Emmanuel Mathias maaruf kama MC pilipili amesem ana ndoto za kuwa mbunge, huku akiwa anafanya harakati nyingi ikiwemo kuutangaza mji wa Dodoma kupitia sanaa ya uchekeshaji jambo ambalo linaongeza hamasa ya kutimiza ndoto yake hiyo.
Amesema kuwa katika ndoto za kuwa mbunge yote yanawezekana lakini anaamini Mungu akipenda au chama chake CCM kikiweza kumteua kuwania nafasi hiyo.
Hata hivyo alisema jamii inapaswa kujua kuwatumia wananchi si lazima uwe umechaguliwa kuwa kiongozi bali hata wewe mwenyewe kuguswa na kuanza kufanya hivyo ni uongozi pia.
”Ndio maana sasa hivi nimeelekeza nguvu zangu katika mji wa Dodoma, ambapo kuna mambo mengi watu wanapaswa kuyajua, yaliyofanywa huko nitakayo yatangaza kupitia shoo ya mc pilipili comedy festival itakayofanyika huko septemba 28 mwaka huu ‘’ alisema
Amesema kuwa katika kuhakikisha watu wa mkoa huo wanapaa ladha zilizokuwa zikiishia Dar pekee ambapo amewapelekea mchekeshaji kutoka nchini Kenya Eric Omond.
Aidha amesema kuwa katika show hiyo atataja mambo 10 ambayo wengine hawayajui yameshafanywa katika mji huo wa kitaifa na kuwezesha kutumika kama fursa katika kujiletea maendeleo huku akiwataja baadhi ya wasanii watakao sindikiza shoo hiyo ni pamoja na Dullyvani, dogo pepe, Ally na Oscar nyerere huku bendi ya TNC ikitumbuiza.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK