Simbachawene Aagiza Kuondolewa kwa Wafanyakazi Wawili wa NEMC Waliopo Bandarini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), George Simbachawene, ameagiza kuondolewa kwa wakaguzi wawili wa Baraza la Hifadhi ya Mazingira (NEMC), waliopo Bandari ya Dar es Salaam, baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu suala la vifungashio vya plastiki vinavyokuja na bidhaa mbalimbali kutoka nje.


Uamuzi huo aliutangaza juzi mbele ya waandishi wa habari baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandari ya Dar es Salaam.

Simbachawene alisema kumekuwa na changamoto nyingi, ikiwemo suala la vifungashio na mifuko mbadala licha ya kanuni kuwa wazi.

Pia alibainisha vifungashio vya plastiki zinavyoruhusiwa na visivyoruhusiwa.

“Kanuni ya 9 imebainisha vifungashio vya plastiki vinavyoruhusiwa ni ile vinavyotumika kwa ajili ya huduma za afya, bidhaa za viwandani, sekta ya ujenzi, sekta ya kilimo, vyakula, usafi na udhibiti wa taka.

“Mnakwamisha biashara za watu, hasa hawa wanaoingiza bidhaa za viwandani kama nguo.

“Ukishaondoa kifungashio kwenye nguo, mpaka ifike dukani kutoka bandari itakuwa nguo kweli?” alisema na kuhoji Simbachawene.

Mbali ya agizo hilo, pia alisema mkanganyiko huo unatokea kutokana na watumishi kukosa weledi wa taaluma au kazi wanazofanya na kusababisha kufanya kazi kwa kubahatisha na kukosa ufanisi katika utendaji kazi wao na kuchangia usumbufu, hasa kwa wafanyabishara wanaoingiza bidhaa mbalimbali za viwandani nchini kutoka nje.

Aidha, Simbachawene aliagiza watumishi kutoka NEMC Kitengo cha Ukaguzi Bandarini kufanya kazi saa 24 wakishirikiana na watumishi kutoka taasisi nyingine za Serikali ili kuongeza nguvu kazi katika ukaguzi wa mizigo inayoingia nchini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad