VURUGU AFRIKA KUSINI: Watu 41 Wakamatwa, Waziri Nigeria Atoa Kauli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Raia kadhaa wa Afrika Ya Kusini wanaoishi katika Jiji la Johannesburg wamechoma moto na kuiba Bidhaa katika Maduka ya raia wakigeni waishio katika Mji huo.

Hata hivyo hali hii imeendelea kutokea kwa raia wa kigeni ambao inasemekana wanawanyima ajira raia wazawa wa Afrika ya Kusini na imesababisha mzozo mkubwa kati ya Waafrika Kusini na raia wa kigeni ambao wanafanya biashara mbalimbali Nchini humo.

Katika Hatua Nyingine Waziri wa Mambo ya nje wa Nigeria Geoffrey Onyeama ametoa Neno kupitia ukurasa wake wa Twitter nakusema kuwa maduka ya raia wa Nigeria yalilengwa na “wahalifu wasio na akili” na akaahidi kuchukua “hatua dhahiri”. Maeneo yaliadhiriwa hapo jana na vurugu hiyo ni Jeppestown, Denver, Malvern na Tembisa.

Baadhi ya taarifa kutoka nchinihumo zinaeleza Watu 41 wamekamatwa na Polisi nchini Afrika kusini kwa madai ya kupora mali na kuchoma maduka ya Wahamiaji kutoka mataifa ya Afrika.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad