Bobi Wine Kiboko Atoroka Ulinzi Mkali wa Polisi Uliotanda Nyumbani Kwake na Kwenda Kushiriki tamasha alilopigwa marufuku

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanamuziki ambaye ni Mwanasiasa, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine amefanikiwa kutoroka ulinzi mkali wa Polisi uliokuwa ukizingira nyumba yake huko Magere

Inadaiwa kuwa kwa sasa Mbunge huyo wa Kyadondo Mashariki anaelekea tamasha lake alilozuiwa kulifanya huko Busabala kwa kutumia Bodaboda

Mapema leo asubuhi Polisi walizingira nyumba ya Bobi Wine ili kumzuia kushiriki katika tamasha lake la muziki liitwalo ‘Osobola ku Independence’ kwa Kiingereza ‘Independet Day Music Concert’

Kwa mujibu wake Bobi Wine amedai kuwa Polisi walianza kuzingira nyumba yake na ukumbi wa tamasha hilo jana usiku akidai Polisi hao ndio walisema hawana uwezo wa kulinda watu huko Busabala

Aidha, Msemaji wa Polisi, Fred Enanga ameeleza kuwa tamasha hilo haliwezi kufanyika kwa sababu Bobi Wine ameshindwa kutofautisha siasa na muziki
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad