AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Schoof amekuwa nchini Rwanda tangu mwaka 2003, akihubiri. lakini mwaka uliopita kituo chake che redio kilifungwa baada ya kuhubiri kupitia kituo hicho kuwa wanawake ni ‘malaya na ibilisi’.
Alikamatwa siku ya Jumatatu, akiwa na mwanaye wakati alipokuwa anataka kuwahutubia wanahabari jijini Kigali akidaiwa kutaka kuishtumu serikali ya Rwanda.
Idara ya uhamiaji inasema, mtoto wake aliachiliwa huru, lakini yeye amefukuzwa kwa sababu, kwanza kibali chake cha kufanya kazi kimeisha na hakuwa na sababu ya kuwa Rwanda maana kituo chake cha redio kilishafungwa.
Kanisa la mhubiri huyo ni miongoni mwa makanisa 700 yaliyofungwa mwezi Februari, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya serikali kuhusu kufungua kanisa.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK