Mtoto achomwa viganja na wazazi kisa kupoteza simu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Jeshi la polisi Kisumu, nchini Kenya, limewatia mbaroni wazazi wa mtoto wa  kiume wa miaka 14, kwa kumchoma moto viganja vya mikono yake kwa tuhuma za kupoteza simu ya mkononi.

Mtoto huyo ni mwanafunzi wa darasa la 8 ambao wanatarajiwa kufanya mitihani ya taifa ya kumaliza shule ya msingi inayoanza jumanne wiki ijayo.

Kwamujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi, Leonard Matete wazazi wote wawili wamehojiwa ili kukamilisha uchunguzi wa tukio hilo.

Jafo awasha moto mwendo wa Halmashauri kufungua akaunti
Mtoto huyo ambaye mama yake alifariki akiwa na umri wa mwaka mmoja, amekuwa akiishi na baba yake na mamayake wa kambo, Rose Akoth.

Imeelezwa kuwa, mama huyo alimzungushia magazeti kwenye viganja vya mikono na kumfunga na kamba kisha kumwagia mafuta ya taa na kumchoma.

Mumewake Onjoro Omuya, alijaribu kufanya kila njia ili kuficha tukio hilo lisijulikane na taarifa za upelelezi zinaeleza kuwa walimkataza mtoto huyo asimwambie mtu kilicho tokea.

Hukumu ya kifo yatolewa, walimuua mwanafunzi kwa moto
Afisa wa polisi wamempeleka mtoto huyo hospitali kwa matibabu zaidi na baada ya hapo watampeleka kituo cha kulea watoto ili ajiandae na mitihani ya taifa wiki ijayo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad