RAIS Magufuli "Vya Bure Vina Madhara yake"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanza. Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema licha ya kuahidi kujenga meli mpya wakati wa kampeni zake mwaka 2015, lakini hakujua fedha atazitoa wapi.

Ametoa kauli hiyo leo Jumapili Desemba 8, 2019 wakati akihutubia mamia ya wananchi wakati wa kuweka mawe ya msingi ya ujenzi wa meli mpya, chelezo na ukarabati wa meli za Mv Victoria na Mv Butiama.

“Hata nilipokuwa naahidi sikujua fedha hizi nitazitoa wapi, kumbe fedha zipo zinachezewa na mafisadi, tuliwabana tukazipata hela hizi,” amesema.

Amesema hata sasa bado mafisadi wapo hawajaisha ila wataendelea kuwashughulikia.

Amesema kinachochelewesha maendeleo ni kutegemea misaada na mikopo. “misaada inatuchelewesha mno, siku za nyuma tulifikiri kuombaomba kunatusaidia ndiyo maana miaka 23 tangu kuzama kwa meli ya MV Bukoba haikuwahi kujengwa kwa sababu ya kutegemea misaada,” amesema.

“Siku zote ukisubiri vya bure kupewa vinamadhara yake, sisi sio masikini tujenge tabia ya kujitegemea,” amesema.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad