Familia ya MSUYA Yapewa Miezi Miwili Kufanya Makubaliano ya Mirathi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imetoa miezi miwili kwa pande mbili za familia za Marehemu Erasto Msuya zenye mgogoro wa kugombea mali zilizoachwa na Bilionea huyo kuondoa tofauti. Mahakama hiyo imezielekeza pande hizo kupeleka mrejesho Mahakamani baada ya muda huo kupita

Jaji wa Mahakama hiyo, Johannes Masara, alisema mahakama imeridhia ombi la Ndeshukulwa Msuya, la kuomba mahakama kuondoa shauri lake la mirathi kwa muda ili familia hizo zifanye mazungumzo

Ndeshukurwa alisema uamuzi wa mahakama umetenda haki, na umezingatia maslahi mapana ya pande zote mbili na anaamini jambo hilo, litamalizika na watoto wa Bilionea Msuya watapata haki yao ya msingi

Ndeshukurwa, mama mzazi wa Bilionea Msuya anapinga Miriamu Mrita, mke wa Msuya kuwa Msimamizi wa Mirathi, akidai kuwa ameshindwa kugawanya mali kwa kipindi cha miaka saba tangu kifo cha Msuya

Miriamu yuko Mahabusu tangu Agosti 2016 akikabiliwa na kesi ya mauaji ya wifi yake, Anet Msuya

Bilionea Msuya aliuawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 20 mwaka 2013 Wilayani Hai, Mkoani Kilimanjaro
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad