Maskini..Mtoto Auawa na Kuchunwa Ngozi..

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Imani za kishirikina zimetawala tukio la mtoto aliyetoweka kwa siku sita na baadaye mwili wake kukutwa ndani ya pagale ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo.

Mwanafunzi huyo wa darasa la pili, Celina Fosi alitoweka siku ambayo alienda mnada wa Mwendapole mjini Kibaha akiwa na shangazi yake ambaye anafanya biashara maeneo hayo.
Waokota chupa waliona mwili wake kwenye jengo ambalo lilikuwa halitumiki na kutoa taarifa kwa wananchi walioenda kuutambua.

Shangazi mmoja wa Celina, Rosmely Haule, ambaye alitoka Dar es Salaam kwa ajili ya kuungana na ndugu zake kumsaka mwanafunzi huyo, alisema baada ya kupata taarifa waliripoti polisi ambao walifika eneo hilo na kukuta mwili wa marehemu ambao waligundua kuwa umekatwa baadhi ya viungo kama sehemu za siri, kitovu, nyama ya chini ya unyayo na kuchuna kichwani sehemu ya nywele,” alisema.
Sehemu nyingine zilizokutwa tofauti kwenye mwili wa marehemu huyo, kwa mujibu shangazi huyo, ni pamoja na kung’olewa meno, kukatwa masikio huku nguo yake ya ndani ikiwa imewekwa mdomoni mwake.

Alisema kuwa pia hali ilionyesha kuwa huenda marehemu alifanyiwa vitendo vya ubakaji kabla ya kuuawa kwa kuwa hali ilionyesha kulikuwa na msuguano eneo alilokutwa amekufa
“Mlangoni nje ya jengo hilo kulikuwa kumepangwa matofali na jirani na mwili wa marehemu tulikuta chupa tupu ya soda, pilipili za mwendokasi, vitunguu, matango na glovu za mipira,” alisema.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi wa Pwani, Wankyo Nyigesa aliyoitoa juzi, jeshi hilo lilipata taarifa hiyo na kufanya taratibu zinazostahili kisha kukabidhi mwili huo kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.

Kamanda Wankyo alisema Jeshi la Polisi linaendelea kuwasaka waliohusika ili hatua zichukuliwe na kutoa wito kwa wakazi wa Pwani kuwa waangalifu na watoto wao.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad