Mataifa yaliyopoteza raia kwenye ndege ya Ukraine yaidai fidia Iran

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mataifa yaliyopoteza raia katika ajali ya ndege ya Ukraine iliyodunguliwa na Iran yameitaka Tehran iwajibike kikamilifu, uchunguzi wa kimataifa uanzishwe na familia za wahanga zilipwe fidia.

Mawaziri wa mambo ya nje wa Canada, Uingereza, Ukraine, Sweden, Uholanzi na Afghanistan wamekutana jijini London katika ubolozi wa Canada.

Mawaziri hao baada ya mkutano wao walitoa taarifa ya pamoja wakiitaka Iran ifanye uchunguzi wa kimataifa utakao kuwa huru na wazi hasa kwa mataifa yanayoomboleza.

Waziri wa mambo ya nje wa Canada Francois-Philippe Champagne amesema wamekutana  kutafuta uwajibikaji na haki kwa wahanga wa mkasa huo na kuongeza kuwa familia za wahanga hao zinataka majibu, jamii ya kimataifa inataka majibu na dunia nzima pia inasubiri majibu na kwamba hawatapumzika hadi watakapoyapata.

Watu wote 176 waliokuwa ndani ya  ndege ya abiria ya Ukraine walipoteza maisha yao wakati ndege yao ilipodunguliwa na kombora muda mfupi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Imam Khomeini mjini Tehran tarehe 8 mwezi huu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad