Mtatiro aagiza wazazi wasiopeleka watoto shule kukamatwa, 50 wadakwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



WAZAZI 50 wamekamatwa na Jeshi la Polisi wilayani Tunduru Mkoa wa Ruvuma, kwa kosa la kutopeleka shuleni watoto wao waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwa kwanza.

Wazazi hao wamekamatwa kufuatia agizo la Julius Mtatiro, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, la kukamatwa kwa wazazi ambao watoto wao hawajaripoti shuleni.

Mtatiro amesema operesheni hiyo ya kukamata wazazi wa wanafunzi wasioripoti shuleni, imeanza baada ya asilimia kubwa ya watoto hao kutoripoti shuleni.

“Siku 14 baada ya shule kufunguliwa, asilimia 71 ya watoto wa kidato cha kwanza walikuwa hawajaripoti shuleni. Baada ya kutoa notisi hii na kuisimamia na kukamata wazazi takribani 50, tumeweza kudahili 60.01% ya watoto ndani ya siku 7 sawa na ongezeko la asilimia 31.01,” ameeleza Mtatiro na kuongeza;

“Katika wiki ianzayo kesho Jumatatu tutaendelea na oparesheni nzito za kuhakikisha watoto wanapelekwa shuleni, siku 7 zijazo tunataka asilimia 80 ya watoto wa kidato cha kwanza wawe wamedahiliwa na wanaendelea na masomo.”

Aidha, Mtatiro amewataka wazazi wasiopelekea watoto wao kufanya hima kutekeleza agizo hilo.

“Kwa hiyo mkianza kukamatwa sitaki kuona mtu anafika ofisi ya mkuu wa wilaya kuja kuleta vifaa, hii ndio operesheni nimeianza hapa. Hilo hamna mjadala. Mjadala wake mlete mtoto shuleni. Na ninataka kuwahakikishia. Kila mzazi atapeleka shuleni mtoto wake,” amesisitiza Mtatiro.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad