AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kamishina Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Ilala, Janeth Magomi, amethibitisha kifo cha Mwandishi wa Habari, Deogratius David, aliyekutwa amefariki Dunia chumbani kwake, maeneo ya Vingunguti Mji Mpya, huku mwili wake ukiwa umeharibika vibaya.
Kamanda Janeth amesema kuwa, taarifa walizipata kutoka kwa majirani, baada ya kupita siku tatu bila kumuona na kusikia harufu kali ikitoka chumbani mwake na ndipo walipoamua kuvunja mlango.
"Mwili wake ulikutwa umelala kifudifudi kitandani kwake ukiwa umeharibika tayari, majirani wanasema waliamua kuuvunja mlango baada ya kutomuona kwa siku tatu, lakini pia kusikia harufu iliyokuwa ikitokea chumbani mwake na wanasema marehemu alikuwa na ugonjwa wa kifafa" amesema ACP Magomi.
Mwili wa marehemu Deoglatius umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK