Mbeya: Mtoto wa Miaka 17 Auawa Baada ya Kujaribu Kupora fedha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mtoto Victor Mwasoro (17), ameuawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kuvamia kibanda cha kutuma na kupokea fedha akiwa na bastola ya baba yake kwa lengo la kupora fedha.

Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki katika eneo la Sae jijini Mbeya na kwamba mtoto huyo alifariki kutokana na kipigo kikali alichokipokea.

Akielezea tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei, alisema mtoto huyo alivamia kibanda cha Sauda Danda akiwa na bastola yenye namba za usajili 00098503 ikiwa na risasi saba.

Alisema baada ya wananchi kumshtukia walimvamia na kuanza kumshushia kipigo kwa kutumia silaha za jadi.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mtoto huyo aliichukua silaha hiyo nyumbani kwao na inamilikiwa na baba yake, wakati anaingia kwenye kibanda hicho kujaribu kuitumia kupora alikuwa ameihifadhi kwenye kifungashio,” alisema Kamanda Matei na kuongeza:

“Baada ya kuokolewa mikononi mwa wananchi waliokuwa wanampiga alikimbizwa katika Hospitali ya Kanda ya Rufani ya Mbeya ambapo alifariki akiwa anaendelea kupatiwa matibabu.”

Kufuatia tukio hilo, Kamanda Matei aliwataka wamiliki wa silaha mkoani humo kufuata sheria za umiliki wa silaha ili zisiingie kwenye mikono ya wahalifu.

Aidha, aliwatahadharisha majambazi wanaotumia silaha kuwa kwa sasa Mkoa wa Mbeya siyo wa kujaribu kufanya matukio ya aina hiyo kwa kuwa jeshi hilo liko makini na liko tayari kukabiliana nao wakati wowote.

Chanzo: IPP Media
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad