CCM Ubungo wamdhamini JPM kurudi Ikulu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ubungo, Lucas Mgonja ameongoza wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, kujaza fomu za kumdhamini mgombea urais wa CCM, Rais Dk. John Magufuli.
Rais Magufuli amechukua fomu ya kuwania tena urais kwa kipindi cha pili jana jijini Dodoma na ameanza kusaka wadhamini 250 mikoani kama utaratibu wa CCM unavyoelekeza.

Taarifa ilitolewa leo na Katibu wa Siasa na Uenezi Wilaya ya Ubungo, Mbaruku Masudi, ilieleza kuwa wajumbe hao wa Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Ubungo , wameshiriki zoezi hilo kwa ngazi ya wilaya,
“Zoezi la udhamini kwa Wilaya yetu ya Ubungo, limehudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Lucas Mgonja, Katibu wa CCM Wilaya Chifu Sylevester Yared pamoja na kamisaa wa chama Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori,” imeeleza taarifa hiyo.

Akizungumza na wajumbe hao, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ubungo, Lucas Mgonja, alisema kuwa hatua hiyo ni heshima kubwa kwao kwani wanaamini Rais Magufuli ni kiongozi mwenye maoni na ataendelea kuifanyia mema Tanzania. 

“Ubungo tunasema kwa kauli moja kwamba Magufuki anatosha, tunamwamini na tumemkubali na tunahkika atatuvusha tena. Miaka mitano ya kwanza hakika ametenda kazi kubwa na kila Mtanzani ni shuhuda nasi Ubungo alitupendelea kwa kuwa na miradi mikubwa ikiwamo Ubungo Inter Change pamoja na barabara ya njia nane kutoka Kimara hadi Kibaha kwetu ni heshima kubwa.

“Si hili tu hata ukiangalia miradi ya maji, ujenzi wa shule na zahanati pamoja na hospitali za wilaya nasi Ubungo ni sehemu ya wanufaika wakubwa wa miradi hii, kwa hakika Rais Magufuli ameitendea haki CCM na aliahidi na ametekeleza kila sekta kama ilani ya chama ilivyoelekeza,” amesema Mgonja.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad