Kapombe aondolewa kikosini Simba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




SIMBA imevimba na usajili mpya wa beki wa kulia, Israel Mwenda ambapo kauli ya Kaimu Msemaji wa Simba Ezekieli Kamwaga, imeanika kwamba tayari usajili wake umeonekana kulipa kwa Didier Gomes, ambapo sasa amelazimika kumweka kando staa wake, Shomari Kapombe, na kutoa fursa kwa kinda huyo.
 

Msimu uliopita, Gomes alionekana kukosa mbadala sahihi wa Kapombe na kulazimika kila mara kumtumia katika kila mechi, baada ya David Kameta ‘Duchu’, kushindwa kuonyesha upinzani aliokuwa akiuhitaji jambo ambalo sasa limezibwa na kinda huyo kutoka KMC.

 

Taarifa ya Kaimu Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga imelijuza Championi Jumatatu kwamba ni wazi sasa kocha wao Gomes ameshusha pumzi yake baada ya kufanikiwa kupata mbadala sahihi wa Kapombe, jambo ambalo mwanzo lilikuwa likimnyima usingizi.

 

“Mashabiki wetu wengi awali walikuwa hawaamini katika usajili wetu wa vijana wenye umri mdogo tuliowapa nafasi msimu huu, ila kiukweli kwa benchi la ufundi sasa hivi linachekelea tu baada ya sajili hizi kuonyesha matunda hasa ukianza na safu ya ulinzi wa kulia, ambapo tumemuongeza Mwenda.

 

“Mwenda ana kiwango bora sana kiasi kwamba amemshawishi kocha, hadi hawazi tena kuhusu Kapombe hata akiumia kama ilivyokuwa mwanzo,” alisema Kamwaga
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad