Samuel Eto Atangaza Kugombea urais wa Shirikisho la Soka Cameroon

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Nyota wa mpira wa soka nchini Cameroon Samuel Eto atangaza kugombea urais wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Cameroon.

Tangazo hilo limetolewa Jumanne katika ukurasa wake rasmi wa Facebook.

"Nimeamua kuchukua uamuzi huu kwasababu ya kuipenda Cameroon na kupenda soka yetu", alielezea Samuel Eto katika taarifa yake.

Aliandika pia, "ni wakati wa kujenga upya mpira wetu".

Baada ya uvumi kadhaa, Samuel ameamua kuwa mgombea wakati kuna utata juu ya marufuku ya uraia mara mbili nchini Cameroon.

Samuel Eto alikuwa raia wa Uhispania wakati alikuwa akicheza Uhispania.

Miongoni mwa masharti yanayotakiwa kuwa mgombea wa urais wa shirikisho la mpira wa miguu la Cameroon, ni marufuku ya kuwa na utaifa wa kigeni.

Samuel Eto ni kigogo wa tatu wa zamani kugombea urais wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Cameroon.

Hata hivyo, bado haijulikani ikiwa ugombea wake utathibitishwa.

Uchaguzi umepangwa kufanyika Desemba 11.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad