AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Nimeiona orodha ya wachezaji, wadau na viongozi wa mpira wa miguu kuelekea tuzo za TFF zitakazofanyika ukumbi wa JK Nyerere
Sina shaka na majina mengi kwenye vipengele vingi ila kwenye kipengele cha MHAMASISHAJI BORA nadhani hapo ndipo nina shida napo
Nimeona jina la Haji Manara, Masau Bwire na Bongo Zozo, YES wawili wa awali sina shida nao ila Hapo kwa BONGO ZOZO anaingia kama MHAMASISHAJI wa timu gani na ameajiriwa kwenye taasisi gani ya mpira wa miguu?
Pasi na shaka niliona nafasi ya Antonio Nugaz kwenye kipengele hicho kwa Kazi aliyoifanya pale Yanga, tena akitambulika kabisa kuwa ni Afisa Mhamasishaji, tunahitaji adubini kung’amua ukweli?
NUGAZ amefanya Kazi kubwa sana hata tukirejea kwenye takwimu za TPLB bado anasimama kwenye mzani wa peke yake na nafasi yake inaonekana Wazi, kwanini tumeificha kwa maksudi?
Sina shaka na ubora wa Bongo Zozo na mapenzi yake kwa mpira ila namuona Kama SHABIKI zaidi Kama Mashabiki wengine nchini ambao labda wangewekwa wote kwenye kipengele chao cha SHABIKI BORA
Namuona Bongo Zozo kama Issa Azam, Jimmy Kindoki, Aggy Daniel au Shabiki yoyote nchini ambaye anasafiri na timu yake kuipa nguvu binafsi nilimuona eneo hilo zaidi na sio Mhamasishaji
To be fair NUGAZ is robbed! Alipaswa kuwa hapo na alikuwa moja Kati ya washindi watarajiwa kwakuwa numbers don’t lie tena kwa takwimu zao wenyewe
Binafsi nimeitazama kwa mlengo huo zaidi
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK