Aliyemuua George Floyd Anakipata Cha MTEMA Kuni Gerezani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Askari Derek Chauvin aliyemuua George Floyd kwa sasa anayaishi matokeo ya matendo yake, akipitia maisha duni gerezani, chini ya ulinzi mkali na uhuru mdogo.


Chauvin amekuwa gerezani kwa takribani miezi 8 katika Kitengo cha Udhibiti wa Utawala, sekta ya makazi yenye vizuizi na usalama mkubwa ndani ya Kituo cha Marekebisho cha Minnesota-Oak Park Heights.


Amekuwa chini ya ulinzi mkali akiwa amezungukwa na kamera za uchunguzi katika kila hatua ya jambo lolote analojaribu kulifanya, huku wafanyakazi wa gereza hilo wakimchunguza kila baada ya dakika 30.


Kwa mujibu wa TMZ mwakilishi wa kituo hicho anasema Chauvin bado ametengwa, bila kupewa nafasi ya kufanya kazi, kuhusika na programu za elimu wala kuwasiliana na wafungwa wengine.


Mwakilishi huyo anaeleza  kuwa sio hivyo tu bali anaoga, anakula, anaenda bafuni na analala kwenye sehemu moja.


Inaelezwa kuwa anapata saa moja pekee kila siku nje ya chumba hicho kwa ajili ya mazoezi. Ingawa maisha ya gerezani ni magumu, lakini inaelezwa ugumu wa anayoyapitia Chauvin umeongezeka mara dufu kwa kuzingatia alichomfanyia marehemu George Floyd Mei 2020.


Mnamo Juni 2021, Chauvin alihukumiwa miaka 22.5  kwa mauaji ya George Floyd. Alikiri kuwa na hatia katika kesi nyingine inayomkabili ya kukiuka haki za kiraia za Floyd.


Hukumu ya kesi hiyo inaweza kumuongezea miaka 25 mingine gerezani mara baada ya kuhukumiwa ambapo atawekwa katika gereza la kudumu

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad