AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Alizaliwa Novemba 23, 1976 katika Kata ya Bulyaga, Tukuyu Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.
Dkt. Tulia alisoma elimu yake ya msingi na sekondari mkoani Mbeya na baadaye mwaka 1998-2003 alisoma sheria Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Mwaka 2005-2007 Dkt. Tulia alifanikiwa kusoma Shahada Ya Uzamivu Huko Cape Town, Afrika Kusini, na
Baadaye alirudi Dar es Salaam na kuwa mkufunzi wa Sheria Chuo Kikuu hadi Mwaka 2014 alipoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba.
Mwaka 2015 alikuwa kati ya wabunge 10 walioteuliwa na Rais kuingia bungeni, na baadaye mwansheria huyu alichaguliwa kuwa naibu spika wa bunge la Tanzania mwaka 2015 hadi hii leo.
Baada ya Januari 6,2022, aliyekuwa spika wa bunge Job Ndugai kujiuzulu, chama cha mapinduzi CCM kilitangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa kumtafuta spika mpya, mchakato ulioanza Januari 11- 15, 2022.
Taarifa ziliripoti kuwa watu 71 walijitokeza kuchukua fomu hizi za kuwania kiti cha uspika ikiwa pamoja na Dkt. Tulia Ackson, ambapo huu leo baada ya kamati kuu ya Halmashauri kuu kufanya kikao Jijini Dodoma wamemteua Dkt. Tulia Ackson kama mgombea wao kwenye nafasi hiyo.
Dkt. Tulia Ackson atatakiwa kujiuzulu unaibu spika wa bunge, jambo ambali litafungua lango la kuanza kwa mchakato wa kumtafuta Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK