George Mpole Kubaki Geita Gold FC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2021/22 George Mpole huenda akaendelea kuwa sehemu ya kikosi cha Geita Gold FC msimu ujao, kufuatia mipango na taratibu zinazoendelea kuchukuliwa na Uongozi wa klabu hiyo ya mkoani Geita.


Mpole alikua anahusishwa na mpango wa kuondoka klabuni hapo, kufuatia uwezo wake wa kupachika mabao kuziamsha klabu kadhaa za Ligi Kuu na kutamani kumsajili katika kipindi hiki cha usajili.


Awali Mshambuliaji huyo alikua akitajwa katika mawindo ya vilabu vitatu vya jijini Dar es salaam (Simba SC, Young Africans na Azam FC), lakini mpango huo unaonekana kufa rasmi, kutokana na viongozi wa vilabu hivyo kufanya usajili wa Washambuliaji wengine kutoka nje ya nchi.


Kocha Mkuu wa Geita Gold FC Fred Felix Minziro aliwahi kusema kuwa, kutokana na kiwango kilichoneshwa na Mpole, huenda wangemkosa msimu ujao wa Ligi Kuu na Michuano ya Kimataifa, kutokana na kuwindwa na klabu nyingi.

 

Hata hivyo Uongozi wa Geita Gold uliwahi kusisitiza kuwa, utapambana kumshawishi Mshambuliaji huyo kuendelea kuwa sehemu ya kikosi chao kwa msimu ujao, kwa kuwa bado wanahitaji huduma yake katika Michuano ya Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Barani Afrika.


Kwenye usiku wa Mastaa Mshambuliaji huyo alipewa tuzo ya Mfungaji Bora na alikua kwenye kikosi Bora cha msimu wa 2021/22.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad