AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Kipolisi Temeke limesema katika ukaguzi wa Mabasi ya Shule yanayobeba Wanafunzi wamebaini mengi yao yana ubovu wa mfumo wa breki na matairi na kuagiza Mabasi hayo yafanyiwe marekebisho.
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Kipolisi Temeke SP. Africanus Sulle amesema hayo wakati akiongea na Madereva wa Mabasi hayo na Wamiliki wa Shule binafsi za Wilaya ya Kigamboni na kuwataka wawe wanayakagua mara kwa mara kuokoa maisha ya Wanafunzi.
"Magari mengi ya ubovu mkubwa kwasababu ni hatarishi wa mfumo wa breki lakini pia tumegundua ubovu mkubwa kwenye matairi, wengi wenu hamnunui matairi mapya, mnanunua matairi yaliyochongwa yanayopatikana chang'ombe mnakuja kubebea Watoto wetu”
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK