Yanga Kwa Hili la Kisinda Mmejikoroga Wenyewe...TFF Mnawaonea

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



TFF INAWEZEKANA INAONEAGA, LAKINI KWA HILI MMEJIONEA WENYEWE!

Tangu jana kumekuwa na lawama kedekede mitandaoni zikielekezwa TFF kwamba wana agenda binafsi na mabingwa wa nchi Yanga SC kwa kitendo chao cha kuzuia usajili wa Kisinda.

Wenye nasaba na Yanga na walio karibu na Viongozi wamejaribu kuichafua TFF kwa kusema INAIONEA Yanga.

Nimejaribu kufatilia jambo hili na nikagundua kwamba Yanga INAJIONEA yenyewe na wapambe wanataka tu kuipaka matope TFF kwa kutotaka kusema ukweli.

Ukweli ni kwamba Yanga SC, Simba SC, Azam FC na Geita Gold FC zote zilishafanya na kumaliza mapema usajili wao wa wachezaji wa Kimataifa na kupewa Leseni zao.

Walifanya mapema kwakuwa usajili wa CAF lazima uwe na Leseni ya ndani kama kiambatanishi ili upate leseni ya CAF kwajili ya Inter clubs competition zao.

Ili kuendana na muda wa usajili CAF, TFF ikafanya UPENDELEO kwa vilabu vyake vipate leseni za ndani mapema na haraka ili wakamilishe usajili wa Kimataifa (CAF).

Yanga SC waliwakilisha majina ya wachezaji wao 12 na wakapewa na leseni za ndani kwajili ya kuambatanisha CAF. Katika hao wachezaji 12 Tuisila Kisinda jina lake halikuwepo.

Baadae Yanga wakaleta jina la Kisinda wakati wameshakamilisha usajili wa wachezaji 12 wa kigeni kama kanuni inavyotaka. Sasa TFF hawawezi kukubali usajili wake kwakuwa atakuwa mchezaji wa 13, lakini hoja pia ya kumtoa yoyote kati ya waliosajiliwa haiwezi kufanya kazi kwenye dirisha hilihili la usajili mpaka labda dirisha dogo.

Kwenye system ya usajili unaweza kuweka wachezaji wa kigeni hata 40, system inapokea kama vigezo vimekamilika. Lakini inawachukua TFF kuwaidhinisha kwa hiyo hoja ya jina la Kisinda kuingia kwenye system kabla ya dirisha kufungwa pia haina mashiko na hoja mfu.

Viongozi wakubali kwamba waliharakisha kupeleka yale majina yale ya mwanzo huku dili la Kisinda likiendelea, labda hawakuwa na uhakika litakuja kukamilika au wamegundua madhaifu wakati washamaliza wachezaji 12 wa kigeni, lakini sio kwamba kuna uonevu popote.

BIN KAZUMARI (The voice of the voiceless)

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad