AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wenyeji wa Kitengela Kenya amelilia asasi za usalama kuwanusuru kutokana na utovu wa usalama unaoendelea kuwakosesha usingizi kila kukicha.
Wenyeji hao wameripoti kuwa majambazi wanaowavamia wana tabia za kiajabu, kwani huwalazimisha kuwapikia mlo kabla ya kuwaibia majumbani mwao.
Mkaaji wa kijiji cha Noonkopir Nchini Kenya alisimulia jinsi simu yake ilivyotwaliwa na kuamrishwa kupika sima na kitoweo cha kuku na majambazi waliomvamia.
Agatha Njogu aliiambia jarida la Nation.africa kuwa alipoendelea kuwapikia wavamizi hao, mmoja wao alikuwa akiwafuatilia yeye na wanao huku wengine wakizidi kuchokora nyumba na kuiba.
"Hawakuwa na haraka. Ni uvamizi uliopangwa kwa makini,” Njogu aliiambia the Nation. Wenyeji wamelaumu ongezeko la visa vya ujambazi, kwa utepetevu wa maafisa wa usalama eneo hilo.
Wanadai kwamba maafisa wa kituo kidogo cha polisi cha Noonkopir, hujitokeza kwa saa chache hata ingawa wanahitajika kwa dharura.
"Tuliamua kuweka kituo kidogo cha polisi kwa sababu ya visa vya uhalifu kwenye mtaa wetu. Ila maafisa kwenye kituo hicho huwekwa kwa saa chache kisha huondoka," mzee wa kijiji cha Noonkopir village Clement Njung'e alinukuliwa akisema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK