Jambazi Apagawishwa na Urembo wa Mwanamke Waliyekuwa Wakimpora, Awaongoza Polisi Mafichoni Mwao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Uamuzi wa jambazi mwenye silaha kutekwa na hisia za mapenzi kwa mwathiriwa wake uliletea genge zima balaa kwani polisi waliweza kuwafuatilia na kuwakamata.

Wakati wa misheni hiyo, Matundura alipagawisha na urembo wa mmoja wa wahasiriwa katika nyumba waliyovamia.


Daily Monitor iliripoti kwamba mshukiwa alikutana na mfanyakazi wa nyumba waliomokuwa wakitekeleza wizii

Tangu mwanzo, misheni ilikuwa ni kuingia tu na kupora mali katika nyumba ya James Wamugunda, mkulima na mfanyabiashara ambaye alikuwa na kisiagi katika boma lake.

Kila kitu kilikuwa kikiendelea kulingana na mpango hadi macho ya Matundura yakatua kwa mjakazi wa nyumba hiyo na akili yake ikapagawa.

Alishindwa kuvumilia akamwomba dada huyo nambari yake ya simu ili wazidi kuwasialiana, naye kipusa akampa bila kusita.

Ulikuwa uamuzi ambao haungewaacha tu katika mashaka bali pia ungemtesa yeye na kundi zima.


Kufikia wakati genge hilo lilikuwa linaondoka nyumbani saa kumi na moja asubuhi iliyofuata, jambazi huyo alikuwa amempenda sana mwanamke huyo.

Matundura na wenzake waliiba bidhaa kadhaa za nyumbani miongoni mwao ikiwa ni cherehani, magunia 10 ya mahindi, simu za mkononi, nguo, viatu na pesa.

Siku iliyofuata, Matundura alimpigia simu mwanamke huyo sio tu kumwomba msamaha kwa yaliyotoke usiku uliopita bali pia kumsihi wakutane naye.



Pia aliendelea na kufichua mahali walipotupa gari walilokuwa wameiba nyumbani.

Msaidizi huyo wa nyumba alikubali kukutana naye katika hoteli ya Choices iliyopo Mchanganyiko lakini alifika pamoja n polisi ambao walimnasa Matundura.

Alikiri kuhusika na wizi huo na kuwaongoza wapelelezi hadi kwenye shamba ambalo walikuwa wamezika silaha na risasi zilizotumika wakati wa wizi huo.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad