Mchungaji Aliyebeba Bunduki Madhabahuni Akamatwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Nigeria. Mchungaji wa Kanisa la House on the Rock, Uche Aigbe ametiwa mbaroni na jeshi la polisi nchini humo kwa kosa la kubeba bunduki aina ya AK-47 wakati wa mahubiri ya Jumapili wakati akitoa mahubiri kuhusu "silaha za kiroho".


Jeshi la polisi limethibitisha kumshikilia mchungaji huyo na ofisa mmoja wa polisi ambaye ndiye mmiliki wa bunduki hiyo.


Kwa mujibu wa kanisa lake, mchungaji Uche Aigbe awali aliomba msamaha kwa tukio hilo.

"Anatambua kwamba hata kwa nia nzuri, kubeba bunduki kuelezea ujumbe wake hairuhusiwi na ameonyesha kujutia kosa hilo," ujumbe wa Kanisa la House on the Rock liliandika katika taarifa yake iliyotoa kufuatia tukio la mchungaji huyo kuingia madhabahuni na bunduki.


Kanisa limeongeza kuwa linapinga aina zote za vurugu na linashirikiana kikamilifu na mamlaka wanapofanya uchunguzi wao kuhusu tukio hilo.


Sheria nchini Nigeria mtu yeyote haruhusiwi kubeba bunduki bila kupewa leseni na Inspekta Jenerali wa Polisi.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad