Mwanasiasa wa Nigeria na mke wake washtakiwa kwa kusafirisha figo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mwanasiasa tajiri na maarufu nchini Nigeria, mke wake na “mhudumu wa afya” wamekutwa na hatia ya njama ya kusafirisha kiungo cha mwili, baada ya kumleta mwanaume wa miaka 21 nchini Uingereza kutoka Lagos.


Seneta Ike Ekweremadu mwenye umri wa miaka 60, mkewe Beatrice, mwenye miaka 56 na Dkt Obinna Obeta mwenye umri wa miaka 50, walishtakiwa kwa kula njama ya kumtoa figo mtu huyo, katika kesi ya kwanza kama hiyo chini ya sheria za kisasa za utumwa.


Ilisikia kwamba kiungo hicho kilikuwa cha binti wa wanandoa hao, Sonia, mwenye umri wa miaka 25.


Mwathirika ambaye ni mfanyabiashara wa mitaani huko Lagos, aliletwa nchini Uingereza mwaka jana kutoa figo katika upandikizaji wa kibinafsi wa kiasi cha fedha cha £80,000 katika Hospitali ya Royal Free huko London.


Mwendesha mashtaka alisema alipewa hadi pauni 7,000 na kuahidiwa fursa nchini Uingereza kwa kusaidia, na aligundua kilichokuwa kikiendelea alipokutana na madaktari hospitalini.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad