Mjane aolewa na wanaume watatu, yumo shemeji yake, wote wanaishi pamoja

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


‘Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Filauni’, Nellie ameitoa ile dhana ya mwanaume kuoa wake wengi bali mwanamke pia anaweza kuolewa na wanaume wengi baada ya kuolewa na wanaume watatu.


Jimmy, Hassan na Danny ndio waume wapya wa Nellie na wameamua kuwa marafiki baada ya kumuoa na kuishi naye kwa pamoja.


Kati ya wanaume hao Hassan ni ndugu wa marehemu mume wake ambaye alibahatika kuzaa naye watoto wawili. Mume wa Nellie alifariki dunia kwa ajali ya gari, hata hivyo mdogo wake huyo alikuwa akiishi nyumbani hapo kama mwanafamilia.


Baadaye alimpata mume wake wa pili na wa tatu katika nyakati tofauti na ambao wote wanaishi nyumba moja na alisema anawahudumia wote na pia imani kwamba hawatamuacha.


Nellie ambaye anafanya biashara ya kuuza magari amesema, "Naitwa Nellie, na mimi ndiye nimeweka rekodi katika kijiji hiki nikiwa na wanaume watatu. Nimeishi na wanaume hawa watatu kama waume wangu kwa miaka mitatu. Nilikuwa na mume ambaye tulikuwa pamoja kwa miaka minane ambaye alikufa katika ajali ya gari,” amesema.


“Baada ya kufariki niliachwa na kaka yake Hassan na tuliendelea kuishi nyumba moja kama ilivyokuwa kabla ya marehemu mume wangu kufariki, hata hivyo alinionyesha upendo na mwishowe nikampenda,” aliiambia Afrimax English.


Akimzungumzia Danny anasema alikuwa amemaliza tu elimu yake na hakuwa amepata ajira alipokutana naye alimwonyesha upendo na kumpeleka nyumbani kwake, ambapo wanaume wengine wawili walimkaribisha.


Nellie alimpata Jimmy akiwa ameketi pekee yake huku akionekana akiwa mpweke, kisha alimuomba wazungumze kwani aliona kama mtu mwenye mawazo mengi.


“Nilihitaji mtu wa kunifariji na kuniambia maneno mazuri, na pia nilihitaji mtu wa kuzungumza naye, aliniambia maisha yake, siku hiyo kila mtu alienda njia yake, lakini tuliendelea kuwa marafiki. Tulikubaliana na historia yetu ya maisha na kuishi kama mume na mke," Jimmy alisema.


Nellie anajivunia kukidhi mahitaji ya waume zake na kujigamba kuwa hawawezi kumdanganya kwa sababu anawapenda wote sawa.


"Kuishi na wanaume watatu kunanifanya nijisikie furaha sana, na ninaweza kuthibitisha kuwa wanaume wangu pia wana furaha kwa sababu wana kila kitu wanachotaka, na nina hakika hawatanidanganya kwa sababu naamini ninakidhi mahitaji yao," Nellie alisema

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad