Rais Ruto Sasa Asema Yuko Tayari Kwa Mazungumzo na Viongozi wa Upinzani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais William Ruto amesema kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo yatakayo mnufaisha Mkenya wa kawaida
Ruto amesema kuwa hatoshurutishwa na kiongozi yeyote kufanya mazungumzo yanayolenga kunufaisha mtu binafsi
Awali kinara wa Azimio Raila Odinga alikuwa ameashiria kuwa mazungumzo yoyote yatafanyika baada ya maandamano ya Jumatatu 20


Rais William Ruto ameonekana kulegeza kamba kuhusu uwezekano wake wa kufanya mazungumzo na viongozi wa upinzani baada ya kusema kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo yatakayoleta manufaa kwa taifa.


Rais William Ruto amesema yuko tayari kwa mazungumzo. Picha Twitter. Chanzo: Twitter
Ruto aliyesema kuwa hatoshurutishwa wala kutishwa ili kukubali mazungumzo alisema afisi yake inakaribisha kiongozi yeyote anayepania kufanya mazungumzo kwa manufa ya wananchi wa Kenya.

"Niko tayari kwa mazungumzo na viongozi wengine iwapo majadiliano yetu yatahusu maisha ya usoni ya taifa hili na yatazingatia sheria na kanuni zilizowekwa kikatiba," Rais alisema wakati wa ibadaa ya maombi Kapsabet.

Rais katika mazungumzo yake alionekana kumnyoshea kidole cha lawama kinara wa Azimio Raila Odinga na kumtaja kama kiongozi anayependa vurugu.


Ruto amesisitiza kuwa hatafanya mazungumzo na vyongozi wenye nia fiche na ambao ajenda yao kuu ni ya kujinufaisha wao binafsi na wala si ya kunufaisha Wakenya.

"Hatutakubali serikali isio na sheria zinazopaswa kufuatwa. Hamtatushia kwa kutupa makaata na kutumia vita ili kutushurutisha na mambo mnayoyafanya basi iwapo tutakubaliana nanyi tutakuwa tunazawadi ukaidi na hilo halitowezekana," Rais aliongezea.
Rais Ruto na viongozi wengine wa Kenya Kwanza siku za hivi karibuni wamekuwa wakishikilia kuwa hawatofanya mazungumzo ya maradhiano haswa na Odinga wakitaja ajenda ya kinara wa Azimio kama ya kibinafsi.

Viongozi wa makanisa akiwemo Askofu wa kanaisa Katoliki Philip Anyolo wamewaomba viongozi hawa wawili kuweka tofauti zao kando na kufanya mazungumzo yatakayohakikisha kuwa taifa linapata utulivu na linakosa migawanyiko.

Kwa upande wake kinara wa Azimio katika mahojiano na runinga ya Citizen alisema kuwa iwapo kutakuwa na mazungumzo ya aina yoyote basi yatafanyika baada ya maandamo ya Jumatatu 20.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad