CUF yafunguka sakata la wanachama 374 kuhama kisa Prof. Lipumba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




CHAMA cha Wananchi (CUF), kimekana kuwatambua wanachama 374 waliotangaza kujivua uanachama, kikidai katika kundi hilo wanachama wake hawazidi 60 na kwamba wengi wao wamekodiwa kwenda kukichafua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Madai hayo yametolewa leo Ijumaa, tarehe 24 Februari 2023 na Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma CUF, Mhandisi Mohamed Ngulangwa, akizungumza na MwanaHALISI Online kwa simu.

“Waliokuwepo eneo husika hawazidi wanachama wetu 60, maana yake ningehesabu ningesema wako 40 au 30 sababu nimefuatilia mkutano wao uliorushwa mubashara (Live) kupitia baadhi ya vyombo vya habari, kuna wakati msema chochote (MC) alisema watu warudishe kadi na idadi ya waliosimama ni wachache sana,” amedai Mhandisi Ngulangwa.

Mhandisi Ngulangwa amedai “tuna ushahidi wako wengine walipewa 5,000 kwa ajili ya kukusanyika hapo ili waonekane wengi lakini kiukweli hakuna wanachama wanaofika 374. Kati ya waliokuwemo kwenye mkutano wengine walionesha kushangazwa kwa kuwa hawakujua kwamba waliitiwa hilo, cha kushangaza wengi, ukumbi ulijazwa na wanachama kadhaa wa Chadema.”


Jana tarehe 24 Februari 2023, wanachama hao wakiongozwa na Shahada Issa, walitangaza kujiondoa CUF huku sababu kuu ya kuchukua uamuzi huo wakidai Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, amekuwa akikiuka katiba, kwa kufanya maamuzi binafsi badala ya kushirikiana na vikao vya chama.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad