Wanaoanza Biashara Kutolipa Kodi Mwaka Mzima

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Ashatu Kijaji amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kibali cha kuruhusu wafanyabiashara wanaoanza biashara kutokulipa kodi kwa kipindi cha miezi sita hadi mwaka moja.


“Rais ametoa kibali, wale wanaoanza biashara kufanya biashara miezi sita hadi mwaka moja ndipo waanze kulipa kodi,” alisema. Alisema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Wilaya ya Kondoa.


Alisema hilo linaonesha ni jinsi gani Rais Samia anawajali wananchi wake. “Ni vyema kila mmoja akauunga mkono juhudi za Rais katika kuwaletea wananchi maendeleo,” alisisitiza. Pia aliwataka wananchi kuachana na mikopo umiza na ile ya kausha damu kwani imekuwa ikiumiza wananchi kutokana na kuwa na riba kubwa.


“Halmashauri zimekuwa zikitoa mikopo ya asilimia nne, wananchi mwende mkope huko. Pia Rais Samia ametoa fedha kwenye Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (Sido) ambapo mikopo hutolewa kwa riba ya asilimia tisa,” alisema. Alisema kuwa mikopo yenye riba kubwa imekuwa ikiumiza wananchi huku wakiwa hawapati faida yoyote.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad