Young Africans Yamlima Barua Kali Mchezaji Feisal Salum

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kwa mara nyingine tena Uongozi wa Young Africans umemwandikia Barua Kiungo kutoka visiwani Zanzibar Feisal Salum Abdallah ‘Fei Toto’ ya kumtaka kurejea kambini kujiunga na wachezaji wenzake.

Young Africans imefanya hivyo, baada ya kukiri kupokea maamuzi ya marejeo ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji kuhusu suala la kiungo huyo.


Taarifa ya Young Africans imeeleza kuwa, baada ya kupokea maamuzi hayo, Uongozi wa Klabu hiyo umemwandikia Barua Feisal Salum kumtaka aripoti kambini haraka iwezekanavyo na kuendelea kuutumikia mkataba wake kama mchezaji wao halali mpaka tarehe 30, Mei 2024, kama ilivyoamuliwa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF.


Hata hivyo taarifa hiyo imesisitiza Klabu ya Young Africans iko tayari kumpokea Feisal Salum na kumjumuisha kwenye kikosi, na kwa kuzingatia sera na utaratibu wa Klabu hiyo katika kuwaongezea mikataba wachezaji wake wanaofanya vizuri.


“Uongozi wa Yanga uko tayari kuendelea na mazungumzo na Feisal Salum Abdallah na wawakilishi wake juu ya kuboresha mkataba wake, kama wataridhia.” imeeleza taarifa hiyo


Katika hatua nyingine Young Africans imeuarifu umma kwamba, iko tayari kumruhusu Feisal Salum Abdallah kuondoka klabuni kwa kuzingatia matakwa ya mkataba na utaratibu wa sheria za uhamisho wa wachezaji zinazotambulika na TFF pamoja na FIFA.


Pia imetoa wito kwa klabu yoyote inayohitaji huduma ya mchezaji huyu, kufuata utaratibu ili kuanza mazungumzo wakati wowote.

Young Africans Yamlima Barua Kali Mchezaji Feisal Salum


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad