Muhudumu wa Ndege Aliyejitoa Uhai wake Kwa Kufa Njaa ili Akutane na Yesu..Inasikitisha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Anaandika Comrade @julius_mtatiro

Kisa cha Betty Ajenta Charles (pichani), kinasikitisha na kutafakarisha sana. Mwili wake umefukuliwa baada ya kufunga mpaka kufa katika sakata linaloendelea nchini Kenya la Mchungaji Paul McKenzie ambaye anawafungisha waumini wake hadi mauti (Fasting to Death) ili wafike mbinguni kirahisi.

Mwili wake ni kati ya miili zaidi ya 90 iliyofukuliwa katika zoezi linaloendelea kwenye jimbo la Kilifi - kijiji cha Shakahola, Pwani ya Kenya. Marafiki na ndugu za Betty wamepata mshtuko mkubwa.


Betty alikuwa mfanyakazi wa @qatarairways, Shirika kubwa la ndege duniani. Aliamua kuacha kazi, akauza ardhi yake kwa Kshs 7,000,000 = sawa na TZS 121,170,000/= na kumkabidhi Mchungaji Paul McKenzie.

Mtoto wa Betty aitwaye Jason alilazimishwa kufunga kwa muda mrefu bila kula hali iliyopelekea aage dunia. Wakati mtoto huyo anafunga hadi kufariki, Betty alikuwa nchini Qatar. Jason alikuwa akiishi na babu na bibi yake kwa wakati huo. Haijulikani ni nani alimruhusu mtoto huyo kufunga hadi kufa.

Baada ya kupokea taarifa za kifo cha mwanaye, Betty alifunga safari kutoka Qatar hadi Kenya kwa ajili ya mazishi ya mwanae. Baada ya mazishi alipotea na hakujulikana alipo tena.

Dada yake anayeishi eneo la Umoja - Nairobi, anasema Betty aliacha barua ya hisia kali kwa mume wake akionesha asingerejea tena milele. Baada ya kuandika barua hiyo Betty aliondoka na wanae wengine kuelekea kwenye Kanisa la Mchungaji McKenzie katika kijiji cha Shakahola, huko Kilifi, kaunti ya Malindi. Alifuta akaunti zake zote za mitandao ya kijamii, akauza vitu vyake vyote, kabla ya kupanda ndege kuelekea Malindi.

Rafiki yake anasema, Betty alimuaga akimjulisha kuwa anaenda kuonana ana kwa ana na Yesu tar 08 Aprili 2023 huko Malindi na hivyo ataondoka Nairobi tar 07 Aprili 2023. Alipofuatilia aligundua Betty alikata ticket ya ndege ya kwenda tu (one way) na siyo ya kwenda na kurudi (round trip).

Katika msako unaoendelea kwenye eneo la ekari 800 linalomilikiwa na Mchungaji Paul Mackenzie, Polisi wamemkamata Mchungaji mwenza anayejulikana kama "Zablon wa Yesu" akiwa anasoma Biblia akieleza yeye angelianza kufunga Juni 2023. A typical KIBWETERE.!
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad