Zoezi Ufukuaji Miili Waliofariki kwa Mfungo Tata Lasitishwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Maafisa wa serikali nchini Kenya, wamesitisha zoezi la kutafuta miili ya watu waliopoteza maisha na kuzikwa katika kijiji cha Shakahola karibu na mji wa Malindi Pwani baada ya mhubiri Paul Mackenzie Nthenge, kuwaambia wasile chakula mpaka wafe ili wakakutane na Mungu.


Waziri wa usalama wa ndani, Kithure Kindiki amesema mpaka sasa miili 90 imefukuliwa, idadi kubwa ikiwa ni ya watoto na wanawake wakati huu zoezi hilo likisitishwa kwa muda kutokana na kukosekana kwa sehemu ya kuhifadhi miili zaidi.


Wanne wafariki kwa mfungo wa kumngoja Yesu, 11 walazwa


Body bags are seen arranged as forensic experts and homicide detectives exhume bodies of suspected members of a Christian cult named as Good News International Church, who believed they would go to heaven if they starved themselves to death, in Shakahola forest of Kilifi county, Kenya April 22, 2023. REUTERS/Stringer

Polisi wafukua miili mingine 10, watano familia moja

Amesema, Mchungaji Mackenzie anastahili kushtakiwa katika Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu ICC kwa ugaidi kwa mauaji ya halaiki, kufuatia mafundisho yake yenye utata yaliyosababisha wafuasi wake hao kufunga hadi kifo na kusema watu wana uhuru wa kuabudu lakini wasitimie hali hiyo kuwaumiza.


Mapema wiki hii Rais wa Kenya, William Ruto, naye alimfananisha Mchungaji huyo na gaidi na kuahidi kuchukua hatua kali kwa wahubiri kama hao, huku tukio hilo limewashangaza Wakenya na kuacha maswali ya kwanini imechukua muda mrefu kubaini tukio hilo.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad