AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mwanza. Mkazi wa kijiji cha Kibitilwa kata ya Ilula Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, Marko Samwel (32) anatibiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi baada ya kujikata na kuondoa kabisa uume wake kwa kutumia kisu.
Samwel anadaiwa kujifanyia kitendo hicho cha kikatili Mei 3 mwaka huu Saa 7 usiku kwa madai kuwa amechoka kuuguza maradhi yanayomsumbua (yamehifadhiwa) kwa zaidi ya miaka mitano.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amesema mwanaume huyo alijikata kwa kutumia kisu kisha kuziondoa kabisa sehemu zake za siri jambo lililosababisha apoteze damu nyingi na kukimbizwa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba kabla yakupatiwa rufaa ya kwenda Bugando anakoendelea na matibabu.
"Amekata uume wake kwa kisu kikali kwa madai kwamba amechoka kuugua, akakimbizwa Hospitali ya wilaya ya Kwimba lakini hali yake ikazidi kuwa mbaya akakimbizwa Bugando,"
"Hali yake inaendelea vizuri na sisi tunaendelea kumsubiria apone kabisa arejee kwenye utimamu wake ili atueleze kwa nini amekata sehemu zake za siri baada ya hapo tutamfikisha Mahakamani," amesema Mutafungwa
Mutafungwa ameitaka jamii kuepuka kuchukua maamuzi yanayoweza kuwaathiri kimwili na kisaikolojia akitolea mfano tukio hilo na kuwataka wenye changamoto kuwahusisha ndugu, wanasaikolojia na viongozi walioko katika maeneo yao.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK