AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Papa Francis amemvua upadri mzaliwa wa Rwanda ambaye amekuwa akihudumu kama kasisi kaskazini mwa Ufaransa kwa takriban miongo mitatu.
Taarifa inayosambazwa mtandaoni iliyotiwa saini na askofu wa Évreux inasema kwamba Wenceslas Munyeshyaka, 64, "anapoteza moja kwa moja haki za ukasisi" na "amezuiliwa" kutumikia "mahali popote" kama kasisi.
Ofisi ya Dayosisi ya Evreux imeithibitishia BBC uhalisi wa taarifa hiyo ambayo inasema kuwa inatokana na agizo la Papa la Machi.
Bw Munyeshyaka, ambaye alikimbilia Ufaransa baada ya mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka 1994, hajazungumzia uamuzi huo.
Alisimamishwa kazi na Dayosisi ya Evreux mnamo Desemba 2021 baada ya kuibuka kuwa amekiri kisheria kuwa baba wa mvulana wa miaka 10.
Bw Munyeshyaka alitawazwa kuwa kasisi nchini Rwanda mwaka wa 1992 ambapo anatuhumiwa kuhusika katika mauaji ya mamia ya Watutsi waliokuwa wamekimbilia kanisani kwake katika mji mkuu wa Kigali wakati wa mauaji ya kimbari.
Mahakama nchini Ufaransa zimemuondolea mashtaka ya mauaji ya halaiki.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK