Rais Samia kuongoza waombolezaji kumuaga Membe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Rais Samia kuongoza waombolezaji kumuaga Membe

Rais Samia Suluhu Hassan, leo Mei 14, 2023 anatarajiwa kuwaongeza mamia ya waombelezaji waliofika katika viwanja kwa Karimjee kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Bernard Membe.


Membe alifariki asubuhi ya Mei 12, 2023 wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam.


Ratiba ya kumuaga Membe ilianza asubuhi ya leo nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam ambako ilifanyika ibada takatifu kabla ya shughuli ya kitaifa kufanyika katika viwanja vya Karimjee.


Viongozi mbalimbali wa Serikali wamewasili katika hafla hiyo akiwemo Naibu Spika Mussa Zungu, Waziri wa Mambo ya Nje, Stargomena Tax na Kamishna wa Uhamiaji, Anna Makakala.


Wapo pia mawaziri na wabunge wa zamani waliowahi kufanya kazi na Membe akiwemo Lazaro Nyalandu, Fenela Mukangara, Stephen Wasira, William Ngeleja na Godbless Lema ambaye ni kiongozi wa Chadema.


Baada ya shughuli ya kutoa heshima za mwisho kukamilika jijini hapa mwili wa Membe utasafirishwa kesho Mei 15, 2023 kuelekea katika kijiji cha Chiponda kata ya Rondo mkoani Lindi ambako maziko yatafanyika Mei 16 mwaka huu.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad