Mnunuzi wa Gari Atoroka na Benz jipya la Milioni 16 wakati wa Majaribio ya kuendesha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Muuzaji wa magari aliyetambulika kwa urahisi kama Manga, amesimulia jinsi mnunuzi mmoja anayejulikana kama Henry alitoweka na gari aina ya Benz lenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16 wakati wa kufanya majaribio ya kuendesha kabla ya kununua jijini Abuja, Nigeria.

Manga alieleza kuwa mfanyabiashara mwenzake wa gari alipeleka gari la kijivu kwa Henry, ambaye alidai kuwa anaishi karibu hapo baada ya kuonyesha nia ya kununua Benz, jarida la TheCable waliripoti.


Kulingana na Manga, Henry alisogea karibu na gari huku mfanyabiashara mwenzake huyo akishuka ili kutoa pesa kutoka kwa waendeshaji wa kituo cha mauzo (PoS) ili kununua mafuta kwenye kituo cha mafuta.

"Walijadiliana N55m [ambacho ni kima sawa na milioni 16 za kenya] kwa ajili ya gari na akasema sawa na akataka kuendesha gari kwa majaribio. Aliendesha gari na rafiki yangu akiwa ameketi upande wa abiria wa gari na wakatoka nje hadi kituo cha kujaza mafuta kilicho karibu na sehemu ya kuosha magari huko Garki ili kununua petroli kabla ya gari la majaribio. "

“Rafiki yangu mara moja alitoka nje ya gari kwenye kituo cha mafuta ili kutoa pesa kutoka kwa opereta wa PoS ili kununua mafuta, jamaa huyo aliondoka na gari. Unajua jinsi ilivyo, hakuna trafiki, hakuna kizuizi huko Abuja na hivyo ndivyo alivyotoroka na gari." Alisema muuzaji huyo.


Msemaji wa Kamanda wa Polisi katika eneo hilo hata hivyo alidhibitisha kupokea ripoti hiyo na kusema kuwa askari polisi wanamfuatilia mtuhumiwa huyo katika tukio hilo sasa linalochunguzwa kama wizi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad