Mchezaji Bigirimana Bado Yupo Yanga, Ishu yake ya Kurudi Imekaa Hivi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Mchezaji Bigirimana Bado Yupo Yanga, Ishu yake ya Kurudi Imekaa Hivi


Mshambuliaji mpya wa Young Africans, Hafiz Konkoni amesababisha kushindwa kupewa nafasi kwa kiungo wa kimataifa wa Burundi, Gael Bigirimana, ambaye alirudi kikosini baada ya kuenguliwa msimu uliopita.

Konkoni, ambaye hana hata majuma mawili mazoezini, aliifungia Young Africans bao moja kwenye ushindi wa 6-1 dhidi ya Friends Rangers, Ijumaa (Agosti 04) iliyopita, akionyesha kuwa mtu sahihi kuziba nafasi ya Fiston Mayele.

Baada ya kuondoka kwa aliyekuwa nyota wa timu hiyo, Mayele, Young Africans iliingia sokoni kutafuta mrithi wake, lakini zoezi hilo likawa gumu kiasi cha mabosi kutaka kumwamini mshambuliaji kinda, Clement Mzize kucheza na Kennedy Musonda.

Lakini bado majadiliano yalikuwa makubwa na kuona kuna ulazima wa kuziba nafasi ya Mayele, wakati huo, Wananchi walikuwa tayari na nyota 12 wa kimataifa wanaotakiwa kikanuni, akiwamo na Bigirimana, ambaye alienguliwa kwa makubaliano katika dirisha dogo la Januari, akimpisha Mamadou Doumbia ambaye pia ameachwa.

Bigirimana alifika kambini Avic Town na kuanza mazoezi akiendelea kuutumikia mkataba wake wa miaka miwili, lakini ghafla alisimamishwa baada ya Young Africans kumpata Konkoni, kwani raia huyo wa Ghana litimiza idadi ya nyota 12 bila Bigi-rimana.

Watu wa karibu na Bigirimana, wameelza kuwa waliamua kukaa chini na Young Africans mwishoni mwa juma lililopita ili kuvunja mkataba jumla, baada ya awali kuambiwa wasubiri.

“Sasa tumechoka, alifanyiwa hivi msimu uliopita na sasa. Tumeamua kuvunja mkataba na tayari viongozi wa Young Africans wanalijua hilo na wanalifanyia kazi,” amesema mtu huyo wa karibu na nahodsha wa zamani wa Bigirimana.

Young Africans inaondoka Dar es Salaam leo Jumatatu (Agosti 07) kwenda jijini Tanga tayari kwa mechi za Ngao ya Jamii, ambapo mabingwa hao watetezi wataanza dhidi ya Azam FC keshokutwa Jumatano (Agosti 09).

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad