Mtangazaji Salim Kikeke Ala Shavu Zanzibar

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) imempa jukumu la kuwa mshauri wa masuala ya habari na uhusiano mtangazaji wa zamani wa BBC Salim Kikeke. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Kikeke ameeleza kuwa jukumu hilo kwake ni kama sehemu ya lengo lake la kurejea nchini kwa kuwa alikuwa nia ya kulisaidia taifa lake.

“Nimerejea Tanzania ili kulisaidia taifa langu kwa hali na mali hii ni fursa ya kipekee kupata nafasi ya kuhusishwa kwenye sera ya uchumi wa bluu ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibae Dk. Hussein Mwinyi.

Hapo awali Kikeke alitabiriwa kuwa ameacha kazi katika Shirika la Utangazaji la Uengereza (BBC) kwa kuwa ameitiwa kazi ya kuwa Msemaji wa Serikali kama ilivyokuwa kwa Zuhura Yunus alipoachaka kazi kwenye shirika hilo hilo la BBC na Serikali ya Tanzania kumteua kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu .

Uvumi huu ulipata nguvu baada ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kumuondoa kwenye nafasi ya usemaji wa Serikali Gerson Msigwa na kumfanya kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni , Sanaa na Michezo lakini uvumi huu ulikwisha pale alipoteuliwa Mobhare Matinyi aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke kushika nafasi ya msemaji wa Serikali.

Kwa Kikeke aliyetabiriwa kushika nafasi ya kulitumikia taifa sasa amekuwa mshauri wa masuala ya habari ZIPA.



----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad