Wachezaji Simba Hali Tete Kigogo wa Simba Afunguka Haya Makubwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Wachezaji Simba Hali Tete Kigogo wa Simba Afunguka Haya Makubwa

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, timu ya Simba SC, imebanwa mbavu nyumbani kwa kulazimishwa sare ya 1-1 na Asec Mimosa ya Ivory Coast.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo kumalizika, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesema wachezaji wa timu hiyo wanaonekana kama wamechoka, hivyo ni lazima usajiri upya ufanyike dirisha dogo ili kuinusuru timu hiyo.

“Simba hawakucheza vizuri hata kidogo wanaonekana wamechoka sana hawana nguvu labda sijui wanawaza michezo ya nyuma, lakini Simba Sc wanahitaji kufanya usajili dirisha dogo, vinginevyo mambo ni magumu.

“Nafasi ya kusonga mbele kwenye michuano hii bado ipo lakini lazima Simba waingie sokoni dirisha dogo tena wafanye usajili mkubwa, la sivyo hatutatoboa,” amesema Rage.

Msimamo

Galaxy – goli 1, pointi 3, nafasi ya 1

Asec Mimosas – goli 1, pointi 1, nafasi ya 2

Simba Sc – goli 1, pointi 1, nafasi ya 3

Wydad goli 0, pointi 0, nafasi ya 4.

Mechi zijazo

Galaxy vs Simba

Asec vs Wydad

Tangu msimu huu umeanza, Simba haijashinda mchezo wowote wa Kimataifa.

Power Dynamo 2-2 Simba SC

Simba SC 1-1 Power Dynamo

Simba SC 2-2 Al Ahly

Al Ahly 1-1 Simba SC

Simba SC 1-1 Asec Mimosac.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad