Sanamu ya Mwalimu Nyerere Yaibu Gumzo Mtandaoni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Huyo sio Nyerere wetu,"

Baadhi ya Watanzania mitandaoni wanasema kwamba sanamu mpya ya kumuenzi mwasisi wao Julius Nyerere haifanani naye.

Sanamu hiyo ilizinduliwa Jumapili nje ya makao makuu ya Umoja wa Afrika katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.

"Najua ishara ni muhimu zaidi lakini sura ya sanamu haifanani kabisa na Mwalimu Nyerere akiwa mzee au kijana," Maria Sarungi anasema kwenye X (zamani Twitter).

Nyerere alikuwa kiongozi wa Tanzania tangu uhuru wa taifa hilo mwaka 1961 hadi 1985.

Alikuwa mwafrika aliyepigania mshikamano wa Afrika na miongoni mwa wapigania uhuru waliopinga utawala wa wazungu wachache kusini mwa Afrika.

Mwaka jana, sanamu ya heshima ya Rais wa kwanza wa Zambia, Kenneth Kaunda, ilibidi kuondolewa baada ya wiki kadhaa za kejeli, huku watu vivyo hivyo wakisema kwamba haikufanana naye.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad