Benchikha hakuwa kocha sahihi kwa Simba - Mchambuzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Benchikha hakuwa kocha sahihi kwa Simba - Mchambuzi

Mchambuzi wa masuala ya soka nchini kutoka kituo cha runinga cha TV3, Boiboi Mkali amedai kuwa aliyekuwa Kocha wa Simba SC, Abdelhak Benchikha hakuwa kocha sahihi kwa timu hiyo.


Boiboi amesema hayo baada ya kocha huyo aliyejiunga na Simba mwishoni mwa mwaka jana (2023) kubwaga manyanga na kuipiga chini timu hiyo akivunja mkataba yeye na wasaidizi wake wawili na kurudi nyumbani kwao Algeria.


"Wakati Benchikha anakuja Simba tulisema sisi kuwa huyu sio kocha sahihi kuifundisha Simba lakini tulitukanwa sana na tulionekana sisi hatujui kitu.


"Benchikha hakupaswa kuja Simba, huyu sio kocha wakuifundusha Simba kwa sababu yeye ni kocha wa mataji na sio kuijenga timu.


"Simba walikuwa wanahitaji kocha wakuijenga timu kwa sababu wakati anakuja Benchikah timu ilikuwa tayari imeshavurugika hivyo walihitaji kocha ambayee ataijenga timu.


"Tatizo sisi tukiongea tunaonekana hatujui kitu lakini huwa tunaonaga mbali kwa sababu tunazijua timu zetu," amesema Boiboi.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad