Klabu ya USM Alger ya Algeria Kufungiwa Mashindano yote ya CAF

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Klabu ya USM Alger ya Algeria Kufungiwa Mashindano yote ya CAF



Klabu ya USM Alger ya Algeria itatozwa faini ya USD $50,000 zaidi ya milioni 129 kwa kutojitokeza kwenye mchezo wa jana Aprili 28, 2024 dhidi ya RS Berkane ya Morocco, mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika uliopaswa kupigwa kuanzia majira ya saa 4:00 usiku kwa saa Afrika Mashariki.

Klabu hiyo pia itatakiwa kuwatalipa RS Berkane USD $15,000 zaidi ya milioni 38 kama fidia ya kulipia gharama za mechi ya kwanza ambayo Berkane walisafiri hadi Algeria na mchezo haukufanikiwa kuchezwa kwa sababu za kisiasa.

Aidha upo uwezekano wa klabu hiyo kutolewa kwenye mashindano yoyote yaliyochini ya Shirikisho la Mpira Afrika (CAF).

Katika mchezo wa jana, USMA walionekana wakitoka katika hoteli waliyofikia huko Morocco tayari kwa kuelekea uwanjani kwaajili ya mchezo huo lakini muda wa mchezo ulipofika hawakutokea ndani ya uwanja.

Awali CAF iliipa ushindi wa mabao 3-0 RS Berkane dhidi ya USMA Alger katika mchezo wa kwanza uliopaswa kuchezwa Aprili 21, 2024 baada ya kushindikana kupigwa kutokana Mamlaka za soka Algeria na serikali kuzuia jezi za Berkane zenye ramani ya Morocco wakisisitiza kuwa hawaitambui ramani ya Morocco iliyopo kwenye jezi za Berkane kwa sababu inajumuisha eneo la Sahara Magharibi na wanaamini kwamba Morocco kudhibiti eneo hilo ni haram.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad