Kocha Gamondi Ataki Utani, Awaandalia SINGIDA FC Kikosi Cha Maangamizi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Gamondi awaandalia Singida FG kosi la maangamizi« NyumaMbele »Comments (0)Listen to Article

WhatsApp

Facebook

Twitter

Email This

Gamondi awaandalia Singida FG kosi la maangamizi

Gamondi awaandalia Singida FG kosi la maangamizi

Kuelekea mchezo wa kesho Jumapili dhidi ya Singida Fountain Gate, Kocha Mkuu wa Young Africans SC, Miguel Gamondi amesema kikosi kipo tayari kwa ajili ya kuendelea kufanya vizuri.


Mchezo huo wa Ligi Kuu ya NBC, unatarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza kuanzia saa 10 jioni.


Gamondi amesema: “Leo jioni tutafanya mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Singida na mazoezi yetu ya leo yatatupa mwelekeo wa wachezaji gani tutaweza kuwatumia kwenye mchezo wa kesho.


“Maandalizi ni ya kawaida kwa sababu tumetoka kucheza juzi na tunajua mchezo wa kesho utakuwa mgumu, lakini tumejiandaa kuhakikisha tunafanya vizuri.


Kocha Gamondi Ataki Utani, Awaandalia SINGIDA FC Kikosi Cha Maangamizi


“Falsafa ya kwanza ya Young Africans SC ni timu na siyo mchezaji mmoja mmoja, wenyewe mmekuwa mashahidi michezo yetu iliyopita tulikuwa na majeruhi, lakini kila mchezaji aliyepata nafasi ya kucheza amefanya kazi yake vizuri.


“Napenda pia kuwapongeza Mashabiki wetu kwa kazi nzuri wanayoifanya kila mahali tunapokwenda kucheza na nilishangaa mashabiki wetu wa Mwanza kwenye mchezo tuliocheza hapa dhidi ya Geita, walikuwa wanashangilia kwa nguvu muda wote wa mchezo, ilikuwa ni kama niko Amerika Kusini, najua kesho watakuja kwa wingi kutupa sapoti.”


Akizungumza kwa niaba ya wachezaji, Gift Fred amesema: “Kwa niaba ya wachezaji wenzangu tumejiandaa vizuri na mchezo wa kesho, kwetu sote kila mchezo ni muhimu na kila mmoja wetu anayepata nafasi kuwa katika kikosi cha kwanza atahakikisha anajituma ili tupate ushindi.”


Mpaka sasa, Young Africans SC inaongoza msimamo wa Ligi Kuu ya NBC kwa kukusanya pointi 52 baada ya kucheza mechi 20.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad