Makalla Arusha Jiwe Gizani Kiaina "Tunasikiliza kero kisayansi bila taharuki"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Makalla Arusha Jiwe Gizani Kiaina "Tunasikiliza kero kisayansi bila taharuki"


Katibu wa Chama cha Mapinduzi- CCM, Itikadi Uenezi na Mafunzo, Amos Makala amesema wametumia njia nzuri isiyozusha tafrani kusikiliza kero za Wananchi wa Mkoa wa Katavi, huku akiitaja njia hiyo kuwa ni ya kisayansi isiyo na kero.


Makala ameyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Kashaulili, katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi na kudai kuwa wataendelea kutumia mfumo huo hata kwa mikoa iliyobaki ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma.


Amesema, hawataishia kusikiliza kero pekee bali hata kutoa majawabu ya kero hizo kwa Wananchi.


Hata hivyo, Makala ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza pindi viongozi wa Serikali ngazi ya Mkoa, Wilaya na Halmashauri wanapo tangaza kusikiliza kero zao na si kusubiri Viongozi wa Kitaifa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad