Yanga Waweka Donge Nono Kumchukua Chama Kutoka Simba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Yanga Waweka Donge Nono Kumchukua Chama Kutoka Simba
Clatus Chama

Taarifa ambazo hazijadhibitishwa zinasema kuwa kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba, Clatus Chama huenda msimu ujao akaibukia katika mitaa ya twiga na Jangwani ambapo ameandaliwa mkataba mnono.

Chama ameshaamua kuondoka katika klabu yake hiyo baada ya kutokuwa na furaha Kwa siku za karibuni hapa ambapo amepitia misukosuko kadhaa ikiwemo kutuhimiwa kuihujumu klabu hiyo pamoja na kupewa makosa ya kinidhamu ambayo uongozi ulishindwa kuthibishisha ingawa walisema hadharani na kumsimamisha mchezaji huyo.

Ikumbukwe kuwa Chama amecheza katika klabu hiyo kwa kiwango kikubwa tangu amejiunga na kufikia hatua ya kuibeba timu hiyo mabegani mwake Kwa kuivusha mara kadhaa katika hatua za juu za michuano ya vilabu barani Afrika akifunga magoli yasiyowezekana.

Mchezaji huyo anaamua kuondoka baada ya kuona hapewi thamani anayostahili katika klabu hiyo aliyoifanyia mambo makubwa tofauti na wachezaji wengine huku mkataba wake ukifikia ukingoni mwishoni mwa msimu huu.

Mwanzoni mwa msimu huu Chama aligoma kujiunga na Kambi ya timu hiyo nchini Uturuki akishinikiza kulipwa stahiki zake na kuingia kwenye mgogoro na viongozi wake mpaka alipolipwa ndipo alijiunga na Kambi ya timu hiyo.

Taarifa kutoka Kwa rafiki wa mchezaji huyo zinasema kuwa kiungo mshambuliaji huyo ameshaamua kuondoka katika klabu hiyo na msimu ujao kuna asilimia kubwa akacheza Yanga japo Azam FC pia imempa ofa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad